Kwa
wafugaji wanaotumia vyakula vyetu wanapewa huduma bure na madaktari wetu,
Wakati wa vifaranga mpaka kuku wanaanza kutaga daktari wetu atafika shambani
kwa mfugaji kila mwisho wa wiki kwa ajili ya kupima kuku uzito na kuangalia
hatari zozote za kimagonjwa au kimanzigira zinaweza kuathiri ukuaji sahihi wa
kuku. Baada ya kuanza kutaga daktari wetu atafika shambani kila baada ya siku
10-14 kuangalia maendeleo ya kuku.
Madaktari wetu watakutengenezea group maalumu la whatap ambalo
litarahisisha upatikanaji wa taarifa za shambani. Wajumbe wa group ni timu ya
madaktari wetu, uongozi wetu, mfugaji pamoja na kijana wa shamba. Kijana wa
shamba atareport kila siku kwenye group utagaji wa siku, kuku wagonjwa, vifo,
ulaji wa chakula na jambo lolote aliloliona kwa siku hyo. Hii inawasaidia
madaktari wetu kupata taarifa haraka za shambani kwa mfugaji kwa ajili ya kutoa
huduma za dharura (Emergence flying doctors service)
Madaktari
wetu pia wanawasaidia wafugaji shughuli mbalimbali za kitaalamu bila malipo
kama vile kuchambua kuku wasiotaga, kufanya tafiti juu za tatizo sugu shambani,
kupeleka sampuli maabara za serikali kama kuna tatizo sugu n.k